INACHO HAMISHA THAMANI YA ULIYE NAE KWA KUONA MWINGINE NI ZAIDI YA ALIYEPO NI MUONEKANO MPYA
Ukweli ni kwamba ULIYE NAE AMA ALIYEPO ndiye wa thamani kubwa kuliko anayeonekana kama mpya, mara nyingi ni namna mtu mpya alivyo jiweka ila kwa uhalisia MAVAZI YANAWEZA KUTENGENEZA UZURI WA MTU ila nguo hizo zikivuliwa huondosha kile wengi hukitazama, Nataka kusema kwamba;-
Kuzoea ni hatua kufikia IMANI na hapo hujengwa kitu kinaitwa KUAMINIWA
Kama hujaaminiwa huwezi kupendwa, mara nyingi watu hawajui kama MTAZAMO MPYA HUFUBAZA IMANI ULIYOIJENGA KWA MIAKA KADHAA na hata kusababisha hali ya utulivu wa FIKRA kutoweka na kuyumbisha maana halisi ya kuwa na uliyemzoea, ndo maana kwa sasa mtu kuharibu alichokijenga ni rahisi bila kujua yeye kuaminiwa huko aliko anzisha uhusiano ni ngumu kuiweka DHAMANA YA UPENDO mwisho kabisa wengi hutamani kurudi walipotoka baada ya kuona hakuna jipya zaidi ya MUONEKANO ambao Pengine ulikuwa wa namna mtu anavyojiweka

Mheshimu aliyekupa nafasi mkajenga DHAMANA YA UPENDO kuliko kuona madhaifu yake na kutaka kutafuta Mwingine, Kuna wakati MAJUTO huja na usipate ufumbuzi, Mapenzi mazuri na yenye radha ni yale unayatengeneza mwenyewe kwa Mtu uliyempa dhamana ya NAFSI pamoja na MOYO wako.

Comments
Post a Comment